Hizi ni hadithi 40 zilizopokelewa kutoka kwa Mtume Muhammad (s.a.w) kupitia kwa masahaba wake. Hadithi hizi zimekusanywa na Imam nawawi kutoka katika vitabu vya hadithi.
Hadithi hizi zimekusanya mafunzo mbalimbali ya Dini, na namna ya kuishi vyema duniani. Pia namna ya kupata radhi za Allah na ni kwa namna gani tutaweza kuokoka na moto.
Kwa ufupi hadithi hizi ni Darasa pekee ambalo linatupasa kulifahamu vyema kwa faida zetu na vizazi. Hadithi hizi ni fupi na ni rahisi kukariri na kujifunza.
Tumeandaa Hadithi hizi kwa lugha ya kiswahili pamoja na kuweka nukuu zake za Asili kwa lugha ya kiarabu. Kama kutatokea makosa kwenye tarjima ya maneno haya matukufu tafadhali tutumie barua pepe.
Tunatarajia radhi za Allah katika kazi hii, na kwako ndugu msomaji tunatarajia dua njema.
Ilisasishwa tarehe
11 Apr 2024