Hii ni App maalum kwa watu wanaopenda kusoma Neno la Mungu kwa lugha mbalimbali ili kuelewa undani na kwa ufasaha. Lugha tatu (3) zilizopo ndani ya App hii yaani Kiswahili, Kihaya na Kingereza zinatoa maelezo mazuri ya kuelewa Neno la Mungu. Si hivyo tu bali pia unaweza kusikiliza Neno la Mungu kwa Lugha zote 3 na kutazama video mbalimbali katika zote 3. Pia unaweza kusoma Biblia hii katika lugha zote 3 kwa wakati mmoja au ukasoma tafsiri moja kwa wakati mmoja kulingana na kuweka utakazozitaka wewe mwenyewe. Ubarikiwe kwa kuchagua App hii.
Ilisasishwa tarehe
13 Mac 2023