Kwa kukupa kazi hii ya kufundisha miongoni mwa watoto, Kanisa limekukabidhi jukumu kubwa na, wakati huo huo, fursa kubwa.
Ni muhimu sana kutangaza Injili kwa watoto, kwa sababu ni amri kutoka kwa Bwana. Isitoshe, watoto wako tayari kupokea habari njema. Wanapenda sana hadithi, na wako tayari kumwamini Mungu.
Ikiwa watoto wanamgeukia Yesu, Kanisa la kesho litakuwa na nguvu. Kwa hiyo, kupitia mafundisho yako, unajenga Kanisa la baadaye.
Labda unahisi kulemewa na jukumu hili? Jua kwamba Mungu yu pamoja nawe - ni yeye yule jana, leo na hata milele. ( Waebrania 13:8 ). Yuko pamoja nawe kama alivyokuwa pamoja na Ibrahimu ambaye hadithi yake tutaisoma mwaka huu.
Hapa kuna usaidizi wa vitendo kwa kazi yako muhimu sana.
Ilisasishwa tarehe
20 Ago 2024